Motifu ya Ukame katika Tamthilia za Janga la Werevu (Mohamed, 2011) na Majira ya Utasa (Arege, 2015)

Mary K. Njeru, John M. Kobia, Dorcas M. Musyimi
{"title":"Motifu ya Ukame katika Tamthilia za Janga la Werevu (Mohamed, 2011) na Majira ya Utasa (Arege, 2015)","authors":"Mary K. Njeru, John M. Kobia, Dorcas M. Musyimi","doi":"10.37284/jammk.5.1.733","DOIUrl":null,"url":null,"abstract":"Suala la ukame limeanza kupata umakini mwingi kwa sababu ya kuongezeka kwa hivi karibuni kwa marudio na makali yake. Mathalani, ni mwanzo wa maafa yanayoaminika kuwa chanzo cha kimsingi cha baa la njaa kwa ajili ya uharibifu wa mazao. Kadhalika, ni kutokana na makali ya ukame katika mataifa mbalimbali Barani Afrika na ulimwenguni kwa jumla, ambapo kumeibuka mijadala mizito miongoni mwa washikadau mbalimbali wa masuala ya kimazingira kote ulimwenguni. Tangu kuvumbuliwa kwa uwanja wa fasihi mazingira miaka ya tisini, waandishi wa kifasihi wamejihusisha katika masuala ya kimazingira ili kuchangia katika utatuzi wa matatizo yanayotokana na uharibifu wa mazingira. Kwa msingi huu, makala hii inajadili namna watunzi wa tamthilia za Janga la Werevu (Mohamed, 2011) na Majira ya Utasa (Arege, 2015) wamesawiri motifu ya ukame kama suala mojawapo la kimazingira kwa lengo la kuweka wazi chanzo na athari zake katika jamii. Makala hii iliongozwa na nadharia ya Uhakiki wa Kiekolojia iliyoasisiwa na Glotferty (1996). Nadharia hii hujikita katika uchambuzi wa kazi za kifasihi kwa kuonyesha uhusiano na utegemeano baina ya binadamu na mazingira. Utafiti ulifanyiwa maktabani ambapo uteuzi wa sampuli wa kimakusudi ulitumiwa kuteua matini teule. Data ya utafiti ilikusanywa kupitia usomaji wa kina wa matini teule. Kutokana na matokeo ya makala hii, ilibainika kwamba, waandishi wa tamthilia teule wamesawiri suala la ukame kwa namna mbalimbali kwa kuangazia chanzo na athari zake. Hivyo, makala hii imethibitisha kwamba, fasihi ya Kiswahili ni nyenzo muhimu ambayo inaweza kutumika katika kuangazia masuala yanayoathiri jamii. Vilevile, utafiti huu ni muhimu kwa washikadau wote wa masuala ya kimazingira Barani Afrika na ulimwengu kwa jumla.","PeriodicalId":112928,"journal":{"name":"East African Journal of Swahili Studies","volume":"139 1","pages":"0"},"PeriodicalIF":0.0000,"publicationDate":"2022-07-04","publicationTypes":"Journal Article","fieldsOfStudy":null,"isOpenAccess":false,"openAccessPdf":"","citationCount":"0","resultStr":null,"platform":"Semanticscholar","paperid":null,"PeriodicalName":"East African Journal of Swahili Studies","FirstCategoryId":"1085","ListUrlMain":"https://doi.org/10.37284/jammk.5.1.733","RegionNum":0,"RegionCategory":null,"ArticlePicture":[],"TitleCN":null,"AbstractTextCN":null,"PMCID":null,"EPubDate":"","PubModel":"","JCR":"","JCRName":"","Score":null,"Total":0}
引用次数: 0

Abstract

Suala la ukame limeanza kupata umakini mwingi kwa sababu ya kuongezeka kwa hivi karibuni kwa marudio na makali yake. Mathalani, ni mwanzo wa maafa yanayoaminika kuwa chanzo cha kimsingi cha baa la njaa kwa ajili ya uharibifu wa mazao. Kadhalika, ni kutokana na makali ya ukame katika mataifa mbalimbali Barani Afrika na ulimwenguni kwa jumla, ambapo kumeibuka mijadala mizito miongoni mwa washikadau mbalimbali wa masuala ya kimazingira kote ulimwenguni. Tangu kuvumbuliwa kwa uwanja wa fasihi mazingira miaka ya tisini, waandishi wa kifasihi wamejihusisha katika masuala ya kimazingira ili kuchangia katika utatuzi wa matatizo yanayotokana na uharibifu wa mazingira. Kwa msingi huu, makala hii inajadili namna watunzi wa tamthilia za Janga la Werevu (Mohamed, 2011) na Majira ya Utasa (Arege, 2015) wamesawiri motifu ya ukame kama suala mojawapo la kimazingira kwa lengo la kuweka wazi chanzo na athari zake katika jamii. Makala hii iliongozwa na nadharia ya Uhakiki wa Kiekolojia iliyoasisiwa na Glotferty (1996). Nadharia hii hujikita katika uchambuzi wa kazi za kifasihi kwa kuonyesha uhusiano na utegemeano baina ya binadamu na mazingira. Utafiti ulifanyiwa maktabani ambapo uteuzi wa sampuli wa kimakusudi ulitumiwa kuteua matini teule. Data ya utafiti ilikusanywa kupitia usomaji wa kina wa matini teule. Kutokana na matokeo ya makala hii, ilibainika kwamba, waandishi wa tamthilia teule wamesawiri suala la ukame kwa namna mbalimbali kwa kuangazia chanzo na athari zake. Hivyo, makala hii imethibitisha kwamba, fasihi ya Kiswahili ni nyenzo muhimu ambayo inaweza kutumika katika kuangazia masuala yanayoathiri jamii. Vilevile, utafiti huu ni muhimu kwa washikadau wote wa masuala ya kimazingira Barani Afrika na ulimwengu kwa jumla.
求助全文
约1分钟内获得全文 求助全文
来源期刊
自引率
0.00%
发文量
0
×
引用
GB/T 7714-2015
复制
MLA
复制
APA
复制
导出至
BibTeX EndNote RefMan NoteFirst NoteExpress
×
提示
您的信息不完整,为了账户安全,请先补充。
现在去补充
×
提示
您因"违规操作"
具体请查看互助需知
我知道了
×
提示
确定
请完成安全验证×
copy
已复制链接
快去分享给好友吧!
我知道了
右上角分享
点击右上角分享
0
联系我们:info@booksci.cn Book学术提供免费学术资源搜索服务,方便国内外学者检索中英文文献。致力于提供最便捷和优质的服务体验。 Copyright © 2023 布克学术 All rights reserved.
京ICP备2023020795号-1
ghs 京公网安备 11010802042870号
Book学术文献互助
Book学术文献互助群
群 号:481959085
Book学术官方微信